mtwara regional referral hospital
(ligula RRH)

Afya ya Uzazi

Kliniki ya kuona wagonjwa wa nje hufanyika mara mbili kwa wiki, kila Jumanne na Alhamis kuanzia saa 2 na nusu asubuhi mpaka saa tisa na nusu mchana.

Kliniki hii inahudumia wagonjwa wote wanaotoka nyumbani au waliopewa rufaa kutoka vituo vya afya vya chini lakini hawahitajiki kulazwa.

Baadhi ya wagonjwa wanaotibiwa kliniki ni wajawazito wenye mimba zisizo na matatizo ya kuhitaji kulazwa, wenye matatizo ya uzazi kushindwa kushika mimba, mimba zinazotoka mara kwa mara, uvimbe katika mji wa mimba (Mfuko wa uzazi), kizazi kutokea njia ya uke, uambukizi katika njia ya uzazi (PID), kupima saratani ya shingo ya kizazi na kuiondoa katika hatua za mwanzo n.k.

Pia kliniki inaona wagonjwa walioruhusiwa kutoka wodini kwa ajili ya kufuatilia maendeleo yao baada ya matibabu.

Kupitia kliniki, wagonjwa hupangiwa upasuaji kwa wale wenye kuhitaji huduma hiyo kama vile upasuaji wa kutoa mtoto (kwa wale wenye sababu za kufanyiwa), upasuaji wa kutoa uvimbe kwenye mfuko wa uzazi (Fibroids), upasuaji wa kutoa kizazi chote, upasuaji wa kutoa uvimbe katika mayai n.k